Posts

Showing posts from November, 2018

UWEZA WA MUNGU JUU YA MAGONJWA NA VYANZO VYAKE

 SEMINA YA NENO LA MUNGU-DODOMA UWANJA WA BARAFU* *MWL.CHRISTOPHER MWAKASEGE* *SOMO: UWEZO WA MUNGU JUU YA MAGONJWA NA VYANZO VYAKE.* *TAREHE  06 MAY, 2018* *SIKU YA KWANZA* *👉 NAMBA ZA SADAKA* https://goo.gl/Z3ozYB *👉LINK YA SEMINA YA LEO YOUTUBE* https://youtu.be/ZU8Q2qbvqPE *👉NAMNA YA KUPATA CD&DVD BONYEZA HAPA* https://goo.gl/tgwoub Hili somo tutaenda nalo kwa siku 8 vile Mungu atakavyotufundisha hatua kwa hatua na tutapata nafasi ya maombi kila siku kadri Mungu anavyotuongoza kwa kadri ya kile Mungu anataka kufanya kila siku. Leo katika kuweka msingi nataka tujibu swali ya _*kwanini MUNGU anataka tujue ya kuwa kuna sehemu ya uweza wake alioutenga mahususi kwa ajili ya kuponya magonjwa na vyanzo vyake?*_ Tutaangalia mistari mitatu na kujibu hili swali kama ifuatavyo:- *Luka 5:17, Luka 4:18 na Matendo 10:38* *Luka 5:17* _“Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijij...